Margaret Rwamba Muraya na Augustine Ndunga Mutwiwa walishtakiwa tofauti katika Mahakama ya Hakimu Mkuu Milimani mnamo Machi 24, 2022 kwa kosa la kughushi vibandiko vya KRA VIP vya kuegesha.
Kufuatia juhudi kubwa za kuhakikisha kwamba hakuna ushuru wa Serikali unaopotea, maafisa wa KRA mnamo tarehe 9 Machi 2022, walifanya msako mkali dhidi ya magari yaliyokuwa na vibandiko vya maegesho ya KRA VIP na kuegeshwa ndani ya Wilaya ya Biashara ya Nairobi. Ilibainika kuwa stika namba NCCA16/HON/2021 na NCCA54/HON/2021 mtawalia zilizobandikwa kwenye magari ya washukiwa hazikuwa halisi na ada ya maegesho haijalipwa. Baadaye washukiwa hao walitambuliwa na kukamatwa.
Wananchi wametakiwa kuendelea kuwa waangalifu na kutoa taarifa za ubadhirifu wa aina hiyo ili kuhakikisha kuwa Serikali inakusanya mapato yanayohitajika.
Kamishna, Uchunguzi na Utekelezaji
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 25/03/2022